Saturday, October 3, 2015

MKUTANO WA KUWATAMBULISHA WAGOMBEA UBUNGE, UWAKILISHI, NA UDIWANI KATIKA TAWI LA RAHA LEO JIMBO LA KIKWAJUNI

Katibu wa Wilaya Mjini Magharib Nd: Fatma Shomari  akifungua mkutano wa kampeni katika tawi la ccm shehia ya raha leo na kuwanadi wagombea kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi uliohudhuriwa na viongozi tofauti wakiomo: Waziri wa fedha wa Tanzania Mh: Sada Mkuya, Wasanii mbali mbali kutokea Tanzania bara kama vile: Mrisho Mpoto, Barnaba na kundi lao. Siku ya tarehe 30/09/2015.
Vile vile alichukuwa nafasi ya kumkaibisha Mwenye kiti wa Jimbo.





Mwenyekiti wa Jimbo la kikwajuni MH: Mvita Kipendera akiwasalimia wana chama wa chama cha mapinduzi na kuwataka wanachama kuwa wamoja katika uchaguzi mkuu wa 25 October na kutofanya makosa na kuipoteza haki yao kwa kumchagua yule asie faa katika dira ya maendeleo.


MH: Mgeni Rasmi: Bi Fatma Said Ali katika mkutano huo alizungumzia masuala ya Amani na Usalama katika kipindi cha uchaguzi na kuwataka wananchi kuwa na Umoja Mshikamano katika kuhakikisha ya kuwa chama cha mapinduzi kinabaki madarakani. Mh: Mgeni Rasmi aliendelea kwa kuwanadi wagombea Ubunge, Uwakilishi pamoja na Udiwani vile vile kuwanasihi na kuwataka Wagombea hao kuwa na Mshikiano ya hali ya juu zaidi ili kukipeleka mbele chama cha mapinduzi.


Wagombea hao wa Ubunge na Uwakilishi wakiwa wanahamu ya kuzungumza machache na wananchi wao wa jimbo la kikwajuni katika tawi la raha leo.

Mh: Mgeni Rasmi alianza na kumkaribisha Mgombea Ubunge Jimbo la kikwajuni:


PICHA 3


Mh: Mgombea Ubunge tiketi ya chama cha mapinduzi Eng: HAMADI YUSSUF MASAUNI ambae pia ni Mbunge Mstaafu wa kipindi cha miaka mitano iliyo pita alifurahishwa sana na ujio wa wanachama wa chama hicho. Alizungumzia juu ya suala zima la ilani ya chama na utekelezaji wake pamoja mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka mitano iliopita.

PICHA 4


ENG: Masauni aliendelea kwa kutoa ufafnuzi juu ya mradi wa maji safi na salama ambao upo katika muendelezo wa awamu ya pili, Vile vile alizungumzia juu ya ajira kwa vijana na kuupa nguvu  mfuko wa elimu wa jimbo ambao unawasaidia Mayatima,  Familiya zisizijiweza na wale ambao wamekosa mikopo ya elimu ya juu. Sihayo tu pia aliahidi kuyazingatia maslahi ya Walimu wa Madrasa na muendelezo mzima wa Mashindano ya Kuhfadhi Qur-an  Tukufu.

Kwa kumalizia aliwataka wanachama na wananchi  wote wapenda maendeleo kuwapigia kura ya ndio wagombea wote wa chama cha mapinduzi na kuwataka kumpigia kura yeye  mwenyewe ili kuendelea na kuwaletea maendeleo katika jimbo lao.

PICHA5+6


Wanachama na wakereketwa wa chama cha mapinduzi walihudhuria kwa wingi katika mkutano huo na kuwaahidi wagombea wote kuunganao katika kila jambo.
 

PICHA 7


MH: NASSOR SALIM (ALJAZIRA) Alitilia mkazo yale yote yaliyo ongelewa katika mkutano huo na kuwaomba wanachama  kuwa kitu kimoja katika kukilinda chama cha mapinduzi, vile vile aliahidi kuitekeleza ilani ya chama cha mapinduzi.


PICHA 8


Naye pia hakuwa nyuma katika suala zima la kuwaombea kura wagombea wote wa ccm kuanzia ngazi ya Urais, Ubunge, Uwakilishi hadi Madiwani na aliwataka wananchi  na wanachama wa jimbo la kikwajuni kummiminia kura zote za ndio.



PICHA 9

Mgeni Rasmi akimkaribisha Mkuu wa Wilaya ya kinondoni na kumtaka awasalimie wagombea na wananchi.


 PICHA 10

Mkuu wa Wilaya wa kinindoni jijini Dar salam ND: Paulo Mkonda akitoa nasaha chache katika mkutano huu.

PICHA 11


akiwauga mkono wagombea hao


PICHA 12


Wagombea wakiwa pamoja na wasanii wakishuhudia kati harakati zilizoendelea uwanjani hapo

PICHA 14


Wananchama wa chama cha mapinduziwakiwa katika burudani ya kushehereka katika mkutano  huo

PICHA 15


Wagombea na wananchi wakiitikia dua kwa pamoja baada ya kumalizika 
kwa mkutano huo.

PICHA 16

…………………………………………………………….

PICHA 17


Wanachama wakiwa katika picha ya pamoja na mgombea ubunge wa jimbo hilo baada ya kumalizika kwa mkutano huo 

No comments:

Post a Comment