Saturday, October 3, 2015

MKUTANO WA KUWATAMBULISHA WAGOMBEA UBUNGE, UWAKILISHI, NA UDIWANI KATIKA TAWI LA RAHA LEO JIMBO LA KIKWAJUNI

Katibu wa Wilaya Mjini Magharib Nd: Fatma Shomari  akifungua mkutano wa kampeni katika tawi la ccm shehia ya raha leo na kuwanadi wagombea kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi uliohudhuriwa na viongozi tofauti wakiomo: Waziri wa fedha wa Tanzania Mh: Sada Mkuya, Wasanii mbali mbali kutokea Tanzania bara kama vile: Mrisho Mpoto, Barnaba na kundi lao. Siku ya tarehe 30/09/2015.
Vile vile alichukuwa nafasi ya kumkaibisha Mwenye kiti wa Jimbo.





Mwenyekiti wa Jimbo la kikwajuni MH: Mvita Kipendera akiwasalimia wana chama wa chama cha mapinduzi na kuwataka wanachama kuwa wamoja katika uchaguzi mkuu wa 25 October na kutofanya makosa na kuipoteza haki yao kwa kumchagua yule asie faa katika dira ya maendeleo.

Thursday, September 24, 2015

EID MUBARAK

Asalam Alaykum Warahmatullah wabarakatu, 
Uongozi wa jimbo la kikwajuni unapenda kuwatakia wananchi wote Eid mubarak.

Sunday, September 20, 2015

BALOZI SEIF AWANADI WAGOMBEA JIMBO LA KIKWAJUNI

Mgeni rasmi ambae pia ni makamo wa pili wa rais wa serikali ya mapinduzi ya zanzibar Mh: baozi Seif ali iddi akitoa maelezo machache katika kuwanadi wagombea wa chama cha mapinduzi katika mkutano wa kwanza uliofanyika tawi la miembeni jitini jimbo la kikwajuni vile vile akielezea baadhi ya changamoto za kijamii zilizofanyiwa ufumlbuzi kama kukamilika mradi wa maji safi na salama.

Mh:balozi akimtambulisha mgombea ubunge kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi    ENG: hamad yussuf masauni pamoja na kumkabizi ilani ya chama cha mapinduzi, 
ENG: Hamad Yussuf MasaunI akitoa maelezo mafupi juu ya kuitumikia na kuilinda ilani ya chama cha mapinduzi.
 akiendelea kwa kauli ya kuwataka wanachama na wakereketwa wa chama cha mapinduzi na wananchi wote pamoja na wapenda maendeleo kwa ujumla kuwataka kumchagua na kumpa kura ya ndio ili amalizie kukamilisha miongoni mwa ahadi alizokwisha kuzianza na kulitumikia jimbo la kikwajuni.

vile vile ENG: Masauni alitoa ufafanuzi juu ya suala la mradi wa maji katika maeneno ambayo yanasumbuliwa na kutoka kwa maji machafu.
aliwaeleza kuwa tayari ameshafanya mawasiliano na mamlaka ya maji (ZAWA) na wako mbioni kulitatuo tatizo hilo. kwani miongoni mwa ahadi zake ni kutatua tatizo la maji katika jimbo la kikwajuni.
 alisema hivyo ili kukamilisha changamoto hizo nilazima wananchi kuweza kumchagua katika uchaguzi mkuu october 2
 MH: Balozi Seif Ali Iddi akiwataka wananchi wa jimbo la kikwajuni kumtambua mgombea uwakilishi katika tiketi ya ccm kuwafikishia matakwa ya wanajamii katika ukumbi wa kutatua matatizo (baraza la wawakilishi) .

mgombea uwakilishi huyo akiwa ni mwingi wa furaha baada ya kupokewa vyema na wanachama wa ccm jimbo la kikwajuni akiahidi kufanya mazuri kwa kuitendea hati ilani ya chama cha mapinduzi.

wanachama na wapenda maendeleo wanaogombania udiwani wakiahidi kuitumikia ccm na kuilinda ilani ya chama baada ya kukabidhiwa rasmi na Mh: Balozi.

Thursday, September 17, 2015

UMOJA NI USHINDI 2015

Ahsanteni sana ndugu wananchi wa Pemba kwa kuja kwa wingi kwenye uwanja wa Chokocho Black Magic kumsikiliza mgombea urais wa Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein leo hii 18.Sept 2015.

 
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dr Ali Mohamed Shein akiwahutubia maelf ya wananchi waliofurika kupita kiasi kwenye Uwanja wa Chokocho Black Wizard kwenye mkutano wa kampeni leo hii tarehe 18 Sept 2015
 
 
 
Mgombea urais wa Zanzibar kwa CHAMA CHA MAPINDUZI dr. Ali Mohamed Shein akizungumza na Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Ng. Vuai Ali mara baada ya kuwasili Uwanja wa Gombani ya Kale leo hii Pemba.
Mgombea Urais Dr Ali Mohamed Shein akiowaonesha Katiba ya CCM wananchi waliohudhuria kwenye mkutano

Wednesday, September 16, 2015

MAENDELEO YA JIMBO LA KIKWAJUNI KATIKA SEKTA YA ELIMU

Nitumeni niendelee kukutumikieni, AHADI KWA VITENDO. Imani, Nia thabiti, Ukweli, Upendo, mashirikiano na mshikamano ndizo nguzo za maendeleo na mafanikio ya jimbo letu La KIKWAJUNI na Zanzibar kwa ujumla. Mabadiliko ya maendeleo huletwa nasi kwa pamoja tunaweza. Yalikuwa ni mashindano ya kuhifadhi Qur-an tukufu yaliyoandaliwa na JUMUIA YA KUINUA JIPAJI VYA KUHIFADHI QUR-AN JIMBO LA KIKWAJUNI.



 Mh: ENG Masauni akiwa anatoa nasaha kwa vijana walio shiriki katika Mashndano ya Qur-an kushoto akiwa na Mh: Jazira  Mwakilishi mteule wa jimbo la kikwajuni 
 

TULIAHIDI TUMETEKELEZA SASA MBELE KWA MBELE

#‎AHADI‬ KWA VITENDO... NIAMINI NIKUTUMIKIE. NILIAHIDI NA NIMETHUBUTU KUTENDA ILA BADO TUNAHITAJI KWENDA MBELE MBALI ZAIDI KWA MAENDELEO YETU, YA JIMBO LETU NA NCHI YETU KWA UJUMLA WAKE.
(MICHEZO)
‪#‎GO‬ FOR KIKWAJUNI.
#GO FOR MASAUNI.


Mh. Hamad Yussuf Masauni akisaliamiana na wachezaji Katika Ligi ya Masauni Cup iliyofanyika katika Viwanja vya mnazi mmoja mjini Unguja


 Mh. Hamad masauni akionesha umahiri wake katika upigaji wa penanti
 
 Mh. Hamad Massauni Akitoa Nasaha Chache Kwa Vijana  katika Fainali ya Ligi ya Masauni Cup