Sunday, September 20, 2015

BALOZI SEIF AWANADI WAGOMBEA JIMBO LA KIKWAJUNI

Mgeni rasmi ambae pia ni makamo wa pili wa rais wa serikali ya mapinduzi ya zanzibar Mh: baozi Seif ali iddi akitoa maelezo machache katika kuwanadi wagombea wa chama cha mapinduzi katika mkutano wa kwanza uliofanyika tawi la miembeni jitini jimbo la kikwajuni vile vile akielezea baadhi ya changamoto za kijamii zilizofanyiwa ufumlbuzi kama kukamilika mradi wa maji safi na salama.

Mh:balozi akimtambulisha mgombea ubunge kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi    ENG: hamad yussuf masauni pamoja na kumkabizi ilani ya chama cha mapinduzi, 
ENG: Hamad Yussuf MasaunI akitoa maelezo mafupi juu ya kuitumikia na kuilinda ilani ya chama cha mapinduzi.
 akiendelea kwa kauli ya kuwataka wanachama na wakereketwa wa chama cha mapinduzi na wananchi wote pamoja na wapenda maendeleo kwa ujumla kuwataka kumchagua na kumpa kura ya ndio ili amalizie kukamilisha miongoni mwa ahadi alizokwisha kuzianza na kulitumikia jimbo la kikwajuni.

vile vile ENG: Masauni alitoa ufafanuzi juu ya suala la mradi wa maji katika maeneno ambayo yanasumbuliwa na kutoka kwa maji machafu.
aliwaeleza kuwa tayari ameshafanya mawasiliano na mamlaka ya maji (ZAWA) na wako mbioni kulitatuo tatizo hilo. kwani miongoni mwa ahadi zake ni kutatua tatizo la maji katika jimbo la kikwajuni.
 alisema hivyo ili kukamilisha changamoto hizo nilazima wananchi kuweza kumchagua katika uchaguzi mkuu october 2
 MH: Balozi Seif Ali Iddi akiwataka wananchi wa jimbo la kikwajuni kumtambua mgombea uwakilishi katika tiketi ya ccm kuwafikishia matakwa ya wanajamii katika ukumbi wa kutatua matatizo (baraza la wawakilishi) .

mgombea uwakilishi huyo akiwa ni mwingi wa furaha baada ya kupokewa vyema na wanachama wa ccm jimbo la kikwajuni akiahidi kufanya mazuri kwa kuitendea hati ilani ya chama cha mapinduzi.

wanachama na wapenda maendeleo wanaogombania udiwani wakiahidi kuitumikia ccm na kuilinda ilani ya chama baada ya kukabidhiwa rasmi na Mh: Balozi.

ENG: Masauni ni mmoja kati ya mpenda vijana na kushirikiana nao katika kukamilisha shughuli za kimaendeleo katika jimbo lake. vijana wakimkubali na kuwanae bega kwa bega.
shamra na shereko shereko zikitanda katika eneo la mkutano huo baada ya kumalizika kwa mkutano huo na kuondoka kwa mgeni rasmi na ndipo eng: hamad masauni akijumuika na vijana wake katika shangwe ya kumainisha ushindi wa kishindo wa tarehe 25 october. vijana wa jimbo la kikwajuni wakionekana kumbeba na kumrusha rusha kipenzi chao na kidume mleta maendeleo katika jimbo lao.
(PICHA NA MOHAMED HEMED: BIZO)

No comments:

Post a Comment